VYAKULA VYA WANGA (CARBOHYDRATES)
Vyakula vya Wanga (Carbohydrates) Je, umeshawahi kujiuliza kwanini; (a) Unakua dhaifu na legelege pale unapokua na njaa? (b) Kwanini unakua hodari na mchangamfu pale unapokua umeshiba? Bila shaka wakati wa njaa hua ni dhiki kubwa sana kwako na haya ndiyo yaliyojiri; Mwili kukosa nguvu,hali inayopelekea kushindwa kufanya kazi,kushiriki michezo. Akili kuchoka haraka na wakati mwingine kushindwa kufanya kazi hali inayopelekea kushindwa kufikiri na kujifunza vizuri. Wengine hupata maumivu ya kichwa. Kinyume cha hayo ni wakati umeshiba unafurahi vizuri hata akili hufanya kazi vizuri hii ni kwasababu mwili umepata nishati kutoka kwenye chakula ulichokula kwa maana nyingine unasema "sasa nina nguvu" . Mwili umendwa na seli ambazo ni mhimili muhimu wa ufanyaji kazi wa mwili.Seli zote za mwili ziwe za misuli,ubongo,ini.. zinahitaji nishati ili ziweze kufanya kazi. Kama seli zitakosa nishati ni wazi kwamba mwili pia hautakua na kazi. Hivyo basi ni muhimu sana...